Mkutano wa Kampeni Nzega:
JK akiri tatizo la maji Nzega, aahidi kuvuta maji kutoka Shinyanga kumaliza tatizo
Mipango imeanza ya kuvuta maji safi na salama kutoka Shinyanga ili kuhudumia wananchi wa Wilaya ya Nzega na vijiji vyake.
Hayo yamesemwa na Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete alipowahutubia maelfu ya wananchi wa nzega kwenye mkutano mkubwa wa kampeni.
Akifafanua mpango huo mkubwa, Mheshimiwa Kikwete alianza kwa kukiri kuwa Nzega imekuwa ikisumbuliwa na tatizo hilo la maji kwa muda mrefu. "Nilipokuja mara ya mwisho niliahidi kulivalia njuga tatizo hili, na sasa mipango imekamilika ili mpate maji kutoka Shinyanga. Na hayataishia hapa, mabomba yatapita hadi Tabora Mjini" alisema Mheshimiwa Kikwete.
Ahadi nyingine alizozitolea ufafanuzi ni usambazaji wa umeme. Mheshimiwa Kikwete alisema japo Nzega Mjini kuna umeme, lakini baadhi ya vijiji bado umeme haujafika. Alisema kabla ya miaka mitano kuisha tatizo hilo litakuwa limeisha.
kwa habari kamili ingia
http://jakayakikwete2010.blogspot.com...
Venezuela and US to work together on mining developments, RodrÃguez says
-
Venezuela's interim president made the announcement after meeting with US
interior minister Doug Burgum at the presidential palace in Caracas.
3 hours ago


No comments:
Post a Comment