Thursday, October 28, 2010

Watanzania wakati umefika wa kutumia faceBook ipasavyo

Watanzania wakati umefika wa kutumia faceBook ipasavyo kwa kuleta Maendeleo Nchini Mwetu. Tukiwa kama Jumuiya ya Watanzania tuishio ughaibuni Tumeamua kutengeneza Special Page kwa ajili ya kujadili mambo muhimu ambayo yanaweza kuleta maendeleo nchini mwetu. hasa , kwa kukosoa na kutoa solutions nini tunapaswa kufanya katika idara zote, ilituwe kama wenzetu USA, CANADA, CHINA , JAPAN , SOUTH AFRIKA ,UK ETC.

Kutokana na uchunguzi tulioufanya % ( asilimia ) Kubwa ya watanzania wamejiunga na mtandao wa Face book. Na tunatumia mda mwingi sana katika hii page kwa siku. Tukiwa kama watanzania tulio na uchungu wa maendeleo tumetengeneza special page iitwayo
DAR ES SALAAM, TANZANIA.

http://www.facebook.com/profile.php?id=100000492651030&ref=pymk#!/pages/Dar-es-salaam-Tanzania/147302971966158

Unachopaswa kufanya ni kujiunga na hii page ( kwa kupofya LIKE)
Kisha utakuwa ushajiunga directly , na utaweza kutoa ushauri wako wa busara katika wall paper ya hii page. Ukiwa na picha ya maeneo yaliopo Nchini mwetu ambayo yanahitaji msaada wa ziada itakuwa ni vizuri zaidi kwani watu ( watanzania wote waliojiunga tunaweza toa ushauri kutokana na swala husika).

Unaweza suggest hii page kwa marafiki zako. wenye busara na hekima.
Ni jukumu letu sote kuleta mabaliko na maendeleo Nchini mwetu. Kuna watu wanadata za kutosha ila wanashindwa njia rahisi yawakuwafikishia walengwa wakati umefika sasa.
Naamini tukiitumia hii page ipaswavyo tunaweza leta maendeleo nchini kwa njia moja au Nyingine.

Busara na hekima yako itachangia kwa asilimia kubwa wakati umefika wa mabadiliko.
Mabadiliko tutaleta sisi Wenyewe. inahitaji uzalendo na kujitolea kwa ajili ya nchi yako
Wenu:
Wadau Ughaibuni

No comments:

Post a Comment