Friday, April 30, 2010

Ras nas kushambulia jukwaa Beirut na Cairo


Mwanamuziki Ras Nas aka Nasibu Mwanukuzi na kikosi chake kikali watashambulia jukwaa katika miji ya Beirut na Cairo kwenye tamasha la Spring Festival 2010 tarehe 14 na 15 mwezi huu.

Bendera ya Bongo itapeperushwa angani na kama wahenga walivyonena, asiye na mwana itabidi aelekee jiwe! Safu ya Ras Nas ina wanamuziki Uriel Seri (Ivory Coast), Chuck Frazier (USA), Karlos Rotsen (Martinique), Larry Skogheim (Norway) na Dag Pierre (Sweden). Wadau habari ndiyo hiyo!


Viongozi watatoka hapahapa
Wadau bado uhitaji wa elimu bora na majengo ni mkubwa sana mana vijijini wanafunzi wanapata elimu kwa tabu sana.Kwa shule kama hii wakati wa mvua hakuna kinacho endelea.




Wadau mambo ya mjini haya






Habari njema kwa wapenzi wa muziki kutoka kwa




MSAFIRI ISMAIL RUSUMO.

Nimetengeneza website www.rusumo.com ambapo wadau wataweza kusikiliza nyimbo mbali mbali za Tanzania kama vile taarab,segere,dance,bongo flava,gospel na nyimbo za kigeni kama vile raggae,za kihindi,pop na nyengine nyingi tu.

Pia kuna dictionary ya kisasa kabisa ambayo ina lugha zote za Ulaya na baadhi ya lugha za Asia,katika dictionary hii baada ya kupata tafsiri ya neno pia unaweza kuona picha za neno hilo kwa kubofya upande wa pili wa Ukurasa.
Kadhalika wadau wataweza kuona hali ya hewa na wakati wa sehem mbali mbali za dunia.
Ukiachana na maneno ya rusumo,mimi binafsi nimetembelea website hii kwa kweli inanyimbo nzuri sana za taarab na aina nyingine nyingi.mdau tembelea ujipatie nyimbo zote za mwambao wa pwana kama unavyojua kuwa hakuna vitu kama hivi kwenye website kwa sasa na brother ndio wa kwanza.

1 comment: