Friday, July 31, 2009


JAMANI UBUNIFU KAZI?
Mambo ya ubunifu wa mavazi unavyo pamba moto huko ukerewe nazani kila mmoja anapajua, haya kazi kwenu wabunifu wetu wa mavazi bongo .

Lady Jaydee a.k.a Manka

ambaye anamiliki bendi iliyoko juu kwasasa Bongo “Machozi Band” inyotumia mtindo wa “Sanya Sanya” amesema anategemea kusimamisha maonyesho yake kwa kipindi cha mwezi mmoja kupisha mfungo wa mwezi wa Ramadhani ambao unakaribia.

Katika waraka wake nipehahabari iliyoupata Jaydee amesema wameamua kusimamisha maonyesho hayo kwa kipindi hicho kutokana na kuwaheshimu na kuwasindikiza waislam wote kwenye mwezi huo.

Akiongeza Jaydee alisema pia atatumia fursa hiyo kwenda likizo baada ya sanya sanya ya muda mrefu toka mwaka uanze bila kupumzika.

“Japokuwa wanasema mlalahoi hana sikukuu, nahitaji hata mwezi mmoja nikatulize akili mahala mbali na nyumbani, ila kwakuwa kwetu mteja ni mfalme nawasikiliza nyinyi maoni yenu na kama mtatasisitiza nipige kazi basi sina budi zaidi ya kutimiza mtakachosema” alisema Jaydee

Jaydee pia aliwaambia watu sababu gani siku hizi anaitwa Manka.

“Unajuwa tulijipa haya majina mimi na wadogo zangu watatu ambao ni Kimario (Mwana FA) Massawe (AY) na yeye mwenye Manka(Jaydee), hii tuliitumia kama inavyojulikana ndugu zetu wachaga walivyo hodari katika kutafuta basi na sisi tunafwata nyao zao” alisema Jide

Thursday, July 30, 2009


JAMANI DUNIA INAMBAMBO,

Mazishi ya namna hii ni alali mbele ya mungu tujaribu kuchangia mawazo wa dau kwasababu wanao fanya mazishi haya sijui kama wanajua umasikini ,



CHOKORAA ANUSA JELAA,

Mwanamuziki wa bendi ya African Stars ‘Twanga pepeta’ Khalid Chuma “Chokoraa”, amefikishwa jana kwenye Mahakama ya Mwanzo Magomeni akikabiliwa na shtaka la kumtukana matusi ya nguoni askari wa usalama barabarani. 


Mwanamuziki huyo anadaiwa kumtukana trafiki wa kike Janeth baada ya kutokea mabishano kati yao. 

Imedaiwa kuwa mwanamuziki huyo alikuwa anashindwa kuendesha gari lililokuwa kwenye foleni, baada ya kuamriwa kufanya hivyo na askari na badala ya kuendesha akamtukana. 

Ilidai kuwa Julai 27 mwaka huu, saa 12 jioni huko Magomeni Mikumi, mshtakiwa alimtukana afande Janeth matusi ya nguoni. 

Imedaiwa kuwa siku hiyo, askari huyo alikuwa anaruhusu magari kwenye foleni, lakini gari la mshtakiwa lilikuwa limesimama badala ya kutembea ndipo alipomfuata na kumuuliza kulikoni. 

Pia, imedaiwa kuwa alimuuliza anakwenda upande gani, kama wa kushoto basi awashe taa zinazoonyesha kuwa anakwenda huko, au aweke gari lake pembeni ili wenzake walio nyuma wapite, lakini mshtakiwa bado aliendelea kusimama. 

Baada ya hapo, ikadaiwa kuwa askari huyo alimuuliza amejifunza wapi udereva, anajifunza au amechukua gari la ndugu yake, ndipo mshtakiwa alipojibu kwa kumtolea matusi. 

Mshtakiwa amekana shtaka hilo na alikuwa bado hajadhaminiwa, lakini baadhi ya wanamuziki wa bendi hiyo, ndugu, jamaa na marafiki wakiongozwa na Mkurugenzi wa ASET, Asha Baraka, walikuwa akifanya harakati za kumuwekea dhamana kortini hapo.

Tuesday, July 28, 2009


KUTOKA MAGAZETI LEO  

WAFANYAKAZI 600 wa Kampuni ya Kupakia na Kupakua Makontena Bandarini (Ticts), jana waligoma kufanya kazi kwa lengo la kuushinikiza uongozi wa kampuni hiyo kutimiza makubaliano sita waliyoafikiana katika mikataba yao ya hiari. 

Pia, walishinikiza kuondolewa kwa Meneja Mkuu wa kampuni hiyo, Neville Bisset na Meneja Utumishi, James Rhombo kwa madai kuwa ndio kikwazo katika kumaliza matatizo yao. 

Wafanyakazi hao walidai kuwa Ticts imeshindwa kutekeleza ahadi ya kuwapandishia ngazi ya mishahara kwa zaidi ya miaka tisa, kuwanyima hisa zao za asilimia tano na kwamba, madereva wa matrekta kufanya kazi kwa zaidi ya saa tisa bila kupata muda wa kula. 

Pia wanapinga kitendo cha wazungu kulipwa fedha nyingi tofauti na wao, kupewa kati ya Sh 5,000 na Sh10,000 kama posho ya ufanyaji kazi katika mazingira magumu kinyume cha makubaliano katika mkataba ambapo walikubaliana kulipwa Sh35,000 na zaidi kwa siku. 

Mbali na posho pia walipinga hatua ya kulipwa Sh75,000 tu badala ya Sh 150,000, inayotokana na upakuaji na upakiaji kwa wastani wa makontena 16 hadi 22 kwa mwezi. 

Dar es Salaam kuanza kuangamiza kunguru weusi 
MKUU wa Mkoa Dar es Salaam, William Lukuvi imewataka wananchi kutoa ushirikiano wa serikali katika kuwaangamiza kungururu weusi waliotapakaa jijini na kuhatarisha maisha ya binadamu na wanyama. 

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana alisema kunguru hao ambao awali waliletwa Zanzibar kwa lengo la kula wadudu waliokuwa wanaharibu zao la karafuu visiwani humo; wanazaliana haraka na sasa wanafanya uharibifu katika maeneo mbalimbali. 

Alisema kunguru hao hivi sasa mbali na kusumbua wananchi wanakula ndege wa asili na kuharibu kizazi chao. 

Kwa upande wa binadamu, alisema kunguru hao wanavamia vyakula pamoja na kuharibu mazingira. 

“Kunguru hawa wameshakuwa hatari kwa maisha ya wanyama na binadamu, kwani wamekuwa wakila ndege wetu wa asili na wanaharibu mazingira na mali mbalimbali kikiwemo chakula na makazi ya watu,"alisema Lukuvi. 

Gazeti la Habari Leo : 
Maiti 19 watambuliwa ajali ya Tanga 
Maiti 19 kati ya 28 wa ajali ya basi la Kampuni ya Mohamed Trans lililogongana uso kwa uso na lori katika eneo la Kwakombo wilayani Korogwe mkoani tanga jana wametambuliwa, 14 wamechukuliwa. 

Maiti 27 wamehifadhiwa katika hospitali ya Mkoa wa Tanga ya Bombo, ambapo maiti mmoja anayefanya idadi ya watu waliokufa kuwa 28, alitambuliwa juzi kwenye eneo la tukio na kuchukuliwa. 

Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Tanga ya Bombo, Dk. Freddy Mtatifikolo, amesema leo kuwa maiti 18 wametambuliwa kwa majina, tisa bado hawajatambuliwa. 

Amesema, kulingana na polisi, abiria waliokuwa wamefunga mikanda ndiyo walionusurika. 

Kati ya walionusurika,wanaume ni 12, wanawake watano na mtoto mmoja wa kike (2), mtanzania mkazi wa Nairobi Kenya . 

Maiti waliochukuliwa hadi leo jioni hospitalini, majina yao na umri ni Hassan Ramadhan (35) wa Manga Handeni, Mkadala Said (32), wa Temeke Dar es Salaam, Ainani Maro (53), Dar es Salaam. 

Mwakyembe ajitoa mhanga, Mongella afyatuka 
Mbunge wa Kyela, Dk Harrison Mwakyembe ameitaka Serikali iufunge mara moja mgodi wa dhahabu wa North Mara ili sumu inayodaiwa kutoka hapo isiendelee kuwadhuru wananchi. 

Mbunge huyo pia ametaka mgodi wa dhahabu wa Geita ufungwe kwa sababu, kwa muda mrefu umekuwa ukitoa kemikali za sumu zinazowadhuru wananchi wa kijiji cha Nyakabale. 

“Kwa nini tuogope wawekezaji kama wakwe” amehoji Mwakyembe na pia kuuuliza kwa nini vifungu vya mikataba havitumiki kuwabana wawekezaji. 

Kwa muda mrefu kumekuwa na madai kuwa mgodi wa North Mara uliopo wilayani Tarime mkoani Mara umekuwa ikimwaga maji yenye sumu katika mto Tigithe. 

Kwa mujibu wa madai hayo, wananchi 21 kati ya waliyoyatumia maji hayo wamefariki dunia, wengine wamekumbwa na matatizo ya kiafya, na pia mifugo 200 imepoteza maisha. 

Gazeti la Uhuru Leo: 
Benki ya Wanawake kuanza kazi rasmi leo 
SERIKALI imesema kuwa Benki ya Wanawake Tanzania itafungua milango yake na kuanza kazi rasmi leo. 

Akitoa kauli ya Serikali bungeni jana, Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto, Margaret Sitta, alisema Benki hiyo itaanza kazi katika jengo la Posta ya zamani Jijini Dar es Salaam. 

Alisema tayari mkurugenzi wa kwanza wa Tawi hilo amepatikana na ni mzoefu katika shughuli za kibenki. 

Waziri Margaret alisema benki hiyo itatoa huduma zote za kibenki, na itakuwa wazi kuwahudumia watu wote bila kujali ni wa jinsi gani au dini gani. 

Waziri huyo alisema malengo makuu ya benki hiyo, ni kukusanya amana kutoka kwa wateja, na pia kutoa mikopo ikiwemo ya ujasiriamali, wanaomiliki biashara ndogo, za kati na kubwa. 

Alisema benki hiyo pia itatoa huduma zingine za fedha ikiwemo kubadilisha fedha za kigeni, huduma za kifedha pamoja na kutoa mikopo na ushauri wa masuala ya kibiashara na uzalishaji, hasa kwa biashara zinazomilikiwa na wanawake. 

Watuhumiwa wa wizi kwa kutumia ATM kizimbani 
RAIA wawili wa Bulgaria wanaotuhumiwa kuiba fedha za wateja wa benki mbalimbali nchini kupitia ATM, wamepandishwa kizimbani na kusomewa mashitaka yanayowakabili. 

Washitakiwa hao, mfanyabiashara Nedko Stanchev (35) na Stela Nedelcheva (23), walifikishwa jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kusomewa mashitaka matatu, baada ya kuahirishwa Alhamisi iliyopita, kutokana na kumkataa mkalimani. 

Upande wa mashitaka, ukiongozwa na Wakili wa Serikali Edger Luoga, ulidai mbele ya Hakimu Mkuu Mkazi Warialwande Lema, kuwa mwezi Julai, mwaka huu tarehe na maeneo tofauti mjini Dar es Salaam, walikula njama za kuibia benki ya Barclays sh. milioni 70. 

Katika shitaka la pili, washitakiwa wanadaiwa kughushi ‘VISA CARD’ namba 4205, 6400, 5789, 1838 zilizotolewa kwa Olga Sokolona kuonyesha kwamba zimetolewa kwao na benki hiyo, huku wakijua si kweli. 

Pia Nedko na Stela wanadaiwa kuiba sh. milioni 14.5 mali ya benki ya Barclays kati ya Julai 14 na 17, mwaka huu. Washitakiwa hao wanaotetewa na Wakili Alex Balomi, walikana mashitaka yote. 
  Printable version Email to a friend



Monday, July 27, 2009


ARI MPYA NGUVI MPYA KASI MPYA

Msemo wa ari mpya nguvu mpya sio kulala kama mdau huyu alielala chini ya mti kinacho takiwa ni kufaya kazi kwa bidii kufaya kazi kukwepa umasikini kuleta maendeleo kwenye taifaletu sio kulala na kutojishugulisha nakituchochote ,


Unakumbuka toka Pwaa ya kwanza kabisa iliyobamba ipasavyo katika anga za Bongo Fleva? 

Ikaja Pwaa Part ngoma iliyosimamiwa na Mtu mzima Lucci ambapo ilimpeleka CP katika Level nyingine kabisa, Level za kimataifa, kwani kiukweli ukiangalia au kusikiliza ngoma ya Pwaa Part2 utakubali ya kuwa CP alifanya kazi ya ziada kuanzia utunzi wake mpaka shooting ya Video yake ilikuwa katika “another Level”, ili kuwapa wapenzi na washabiki wake mautamu zaidi na kuonyesha nini amekusudia mchizi muda si mrefu ataachia songi lake la Pwaa Part3. 

Bila kuweka kazi ni nani na nani watakaokuwa wamesimama kwenye ngoma hiyo, CP wakati anaongea na Nipehabari alisema ya kuwa huo ni mwendelezo wa ngoma yake hiyo ambapo kwa madai yake mwenyewe mchizi amesema anatarajia kuifanya tofauti zaidi, na habari za ndani zinasema kuna Pwaa kibao zinakuja, sasa mpenzi na mshabiki wa CP na muziki wa Bongo Fleva kwa ujumla kaeni mkao wa kula kumsikiliza na kumuona jamaa ubunifu zaidi na zaidi.

Miss Temeke Kujulikana Jumamosi

Shindano la kumfuta kisura wa wilaya ya Temeke ambaye ataiwakilisha wilaya hiyo kwenye mashindano ya Kitafaifa ya Miss Tanzania 2009 linatarajia kufanyika mwishoni mwa wiki hii katika ukumbi wa TCC Chang’ombe. 


Akiongea na Nipehabari mratibu wa shindano hilo toka kampuni ya BMP Benny Kisaka alisema mipango yote tayari kwa ajili ya mtanange huo. 

“Kama tulivyowaarifu shindano lenyenyewe litakuwa siku ya tarehe 31 mwezi huu yani Jumamosi ijayo ambapo warembo watapanda jukwaani kumtafuta mwakilishi wa Miss Kinondoni kuelekea Miss Tanzania hapo baadaye, zaidi ya shindano hilo pia kutakuwa na burudani toka kwa Marlaw, Twanga Pepeta na burudani nyingine nyingi tu” alisema Benny 

Temeke mojawapo ya wilaya ambazo zimewahi kufanya vizuri katika mashindano hayo itataka kujiwekea mwiko wa kusubmbuliwa na Kinondoni ambao ndio wababe wa mashindano hayo kwa kupeleka mwakilishi mwenye sifa na vigezo. 

Mazoezi ya washiriki yanaendelea chini ya mwalimu wao Lona Swai, Nyamwela na wengine. 

Kiingilio ni Tshs 50,000/- kwa VIP, wadhamini wa Reds Miss Temeke mwaka huu ni Mariedo Boutique, Valley Springs, Ally Rhemtullah, Screen Masters, 88.4 Clouds FM na wengine.

Friday, July 24, 2009


SEXY SUMMER PARTY WASH,DC,AUGUST 1st
KAMPUNI YA "DMK GLOBAL PROMOTIONS" YA MJINI WASHINGTON DC INAWALETEA THE SECOND ANNUAL **SEXY SUMMER PARTY** LEO - BIRTHDAYS CELEBRATION.
THIS TIME BIGER & BETTER,
FLOOR ZOTE MBILI ZITAFUNGULIWA PAMOJA NA NJE KOTE.

DJS JUU 2 DJS NA CHINI- 2DJS -JUMLA- 4 DJS

4 BIRTHDAYS TAYARI ZIMEISHA RESERVE WITH TOTAL OF 200 GUESTS.

DOORS OPEN AT 8:00PM

LADIES FREE UNTIL 10:30PM

DRESS CODE- FASHIONABLY-JIPIGILIE UPENDAVYO SIUNAJUA SUMMER TIME-MRADI USIVAE,KAPTULA NA TIMBERLAND.

MUZIKI NA - DJ MAC,DJ ACE,DJ AMAZ-95.5WPGC FM&THE ONE & ONLY CAT DADDY DJ JOE 93.9WKYS
LADIES FREE B4 10:30- LAKINI GENTS FREE B4 10:30 UKIWA KWENYE GUEST LIST
MAELEZO ZAIDI AU TO BE ON THE GUEST LIST PLEASE CALL-
DMK @ 301-661-6207 .
AU RESERVE TABLE AU GUEST LIST AT
RSVP@DMKPROMOTIONS.COM
WEB-
WWW.DMKGLOBALPROMOTIONS.COM
GALLERY LOUNGE
1115 EAST WEST HIGHWAY
 SILVER SPRING,MD
K A R I B U N I W O T E.

President Jakaya Kikwete presses a knob to inaugurate the Seacom International undersea fibre optic network at an occasion held in Dares Salaam yesterday. Left is Science, Technology and Communication minister Peter Msola.

The submarine cable launched yesterday in Dar es Salaam is expected to revolutionise internet and telecommunication services in the country by improving efficiency and easing the current costs by over one third, it was announced yesterday.

President Jakaya Kikwete, who graced the glamorous function to launch the SEACOM Ltd’s optic fibre cable at Kunduchi area on the shores of the Indian Ocean, highlighted the good news in his speech to officially kickstart the project.

“This project comes with many social and economic benefits ….But; in short, this tiny, but powerful cable almost literally bridges the digital divide. It will empower Tanzanians and other East Africans to become fully digital citizens of the 21st century. It is the ultimate embodiment of modernity and global connectivity,” he said.

He noted that until yesterday, the Eastern African coast was the longest coastline in the world without optic fibre cable connection to the rest of the world. “Today, this is history,” he declared.

He said the arrival of the cable before the end of the first decade of the 21st century signals the beginning of a new era in the telecommunications sector, particularly data services, in the East African region.

However, he said the landing of the cable on Tanzanian shores could only be useful if there was a terrestrial link to pull it further inland to the masses of users.

“I am happy to let you know that, we already have some existing network with Tanzania Electricity Company (Tanesco), Tanzania Railways Limited and Songo Songo Gas Pipeline. But, we have been working on a wider network to cover the whole country,” he said.

Kikwete added that the government has secured part of the financing and work has started of laying the National Optic Fibre Cable (OFC) network to serve as the information and communication technology backbone.

Part of the network, he said, will become operational this year, covering a distance of 10,674 kilometers, including the pre-existing cable network.

“As we celebrate here today, construction work for this cable is ongoing from Singida towards Shinyanga, Mwanza, Rusumo (Rwanda Border), Mtukula (Uganda Border) and Kabanga (Burundi Border),” he said, adding: “Through our terrestrial cable network, we want to move this cable fast to our East African neighbours of Uganda, Rwanda and Burundi.”

He said the SEACOM system test performed to connect the Mbezi landing station to sites within Dar es Salaam has shown good performance.

“I have also been made to understand that, in a few days to come, it will be ready for use in Dodoma including the University of Dodoma, Prime Minister’s Office, Regional Administration and Local Government, Ministry of Communications Science and Technology and the Parliament. In this regard, we are ready to use the SEACOM landing station capacity and also ready to work with you to position Tanzania as an important Regional ICT player,” he said.

He said the coming of SEACOM submarine cable system to Tanzania would enhance the nation’s capacity to create digital opportunities to areas with coverage as well act as a catalyst to reduce the digital divide in the under-served and un-served areas.

“My desire is to ensure that the opportunities provided by the SEACOM sub-marine cable system reach all Tanzanians irrespective of their geographical location or economic status,” said Kikwete.

However, he cautioned: “While we are celebrating the lighting of SEACOM cable here today, I wish to bring to your attention the importance of taking into account security and safety measures.”

He said there was need to work towards devising strong systems for protecting information at all levels: individual, group, institutional, national and global levels.

Earlier, SEACOM Chief Executive Officer, Brian Herlihy said that the submarine cable would help Tanzanians, particularly in education, health and economic sectors.

He said for the economic sector, the new system was set to change by 100 percent the market system with farmers within the country being able to advertise their products to the developed world through the internet.

“The system is very fast and cheap, therefore local farmers from rural areas will be able to sell their products by advertising them through SEACOM,” said Brian.

Said Abdallah, Chief Operating Officer of an international Telecommunication gateway company, Six Telecoms Company Ltd, said that the introduction of the undersea fibre cable would help the telecommunication middlemen in the country cut down costs, thereby reducing consumer prices for communication services to end users.

Abdallah said that the technology coming with the submarine cable, which replaces the use of satellite, would help in speeding up international communication by around 70 to 80 per cent.

SOURCE: IPPMEDIA

Thursday, July 23, 2009



Tuma neno klexmusic kwenda namba 15551 Nautapata Club Event Shows za Bongo Flava na Rumba pamoja na Part zinatotokea ndani ya Dar kila week na garama ya kujiunga ni Sh/300


SWAHILI FASHION WEEK 2009

The annual Swahili Fashion Week 2009 is to be held during the month of November 2009 in Dar es Salaam , Tanzania . With 12 Tanzanian Designers Showcasing last year, including Those from Zanzibar and Mwanza, This year More designers are to be featured from all over Tanzania and neighbouring Swahili speaking countries. The preparations are underway this year, to create a Three Day of...
he annual Swahili Fashion Week 2009 is to be held during the month of November 2009 in Dar es Salaam , Tanzania . 

With 12 Tanzanian Designers Showcasing last year, including Those from Zanzibar and Mwanza, This year More designers are to be featured from all over Tanzania and neighbouring Swahili speaking countries. 

The preparations are underway this year, to create a Three Day of Fashion Galore, Gallantry. Glitz and Glamor of what best East Africa has to offer. 

The participation is not limited to Fashion designers only, but is open to Accessory, jewellery, handbags and Shoe Designer also. Swahili Fashion Week is open to all designers. Both emerging and established, from Swahili Speaking countries. 

To be invited to Showcase at this Annual Event, the requirements are : 
- A brief Updated (as of 30 June 2009) Profile / Biography 
- Minimum three Images of your work which best portray your Creativity. 
- Why you should be invited to showcase at the Swahili Fashion Week 2009? 

The Above requirements can be electronically be E-mailed to info@swahilifashionweek.com 

or can be sent via Swahili Fashion Week, P.O.BOX 10684 Dar Es Salaam, Tanzania, Not later than 31 July 2009. (Please Strictly Adhere to the Deadline) 

Swahili Fashion week is the dawn of a new era, initiating a dynamic and promising platform for the fashion industry in Tanzania , The Swahili Fashion Week is geared towards being the most sought out after Fashion platform, in Eastern Africa for the International market. 

Swahili Fashion week is a platform for designers, both fashion and accessory, from Swahili speaking countries to showcase their creativity, market their art and networking with clients all aimed at Promoting Fashion as an income generating, Job creating industry emphasizing the “Made in Tanzania” patriotism. 

The successful Inaugural Swahili Fashion Week 2008 took place on 5 & 6 of November 2008 in Dar es Salaam under the meticulous choreography and direction of Jan Malan Umzingeli (http://www.janmalan.com) from South Africa . 

Not only did it showcase Tanzanian Designer and Models but also the Finalist of M’Net Face of Africa 2008. 

CONTACT PERSON : Mr. Hamis Omary 
TELEPHONE NUMBER : +255 78 774 7918 
EMAIL ADDRESS : media@swahilifashionweek.com 
WEBSITE URL: http : //www.swahilifashionweek.com

Wednesday, July 22, 2009


Channel O Awards 2009

AY, Mwana FA pamoja na Black Rhino, watatuwakilisha katika kinyang’anyiro cha tuzo za muziki za Channel O mwaka huu nchini Afrika Kusini.


Kutoka Gazeti la Habari Leo 
Wazungu ‘waiba’ mamilioni ATM 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata raia wawili wa Bulgaria wanaodaiwa kuiba zaidi ya sh milioni 70 katika mashine za kutolea fedha, ATM jijini Dar es Salaam. 

Watuhumiwa hao, Nedko Stanchen(34) na Stella Nedekcheva(23) walikamatwa mwishoni mwa wiki jijini humo baada ya polisi kuweka mtego wakishirikiana na benki ya Barclays wilayani Kinondoni. 

Kamanda wa Polisi wa kanda hiyo, Suleiman Kova amesema leo kuwa, vijana hao wanadaiwa kuhusika katika mtandao wa wizi wa fedha katika mashine za ATM za benki mbalimbali. 

Amesema, polisi waliweka mtego baada ya mfanyakazi wa benki ya Barclays kugundua kuwa kuna vifaaa vilikuwa vimewekwa katika mashine za ATM. 

Amewaeleza waandishi wa habari kuwa, mfanyakazi huyo alikuwa anafanya usafi, na kwa mujibu wa Kova, vifaa vilivyowekwa kwenye mashine za ATM ni kamera na kifaa cha kunakili taarifa za wateja zilizomo kwenye kadi za ATM. 

Wabunge wataka TTCL ilipwe madeni 
WABUNGE wameitaka serikali kuilipa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) deni lake la Sh bilioni 9.2 inazodai wizara na taasisi za umma. Wamesema sasa hivi TTCL inakabiliwa na ukata wa fedha, hivyo serikali ilipe deni lake hilo ambalo ni la hadi Juni 2005 na riba na kuisaidia kampuni hiyo kujikwamua kutokana na hali hiyo ngumu. 

Akisoma maoni ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Ephraim Madeje kwa niaba ya Mwenyekiti wake, Mohamed Missanga, alisema mbali na deni hilo, pia serikali iinusuru kampuni hiyo kwa kulipa madeni yake yote mapema . 

Mionzi yadaiwa kuvunja ndoa, kuua paka Mererani 
ZAIDI ya wafanyakazi 700 wa mgodi wa kuzalisha madini ya vito vya tanzanite, unaomilikiwa na Kampuni ya Tanzanite One, uliopo Arusha wanadaiwa kuathirika na mionzi iliyotokana na mashine ya X-ray ya kuwakagua iliyopo mgodini hapo. 

Baadhi ya waathirika hao wamedaiwa kupata matatizo sehemu za siri na kusababisha kuachwa na wake zao. Tuhuma hizo nzito dhidi ya kampuni hiyo inayomilikiwa na wawekezaji wa Afrika Kusini, zilitolewa jana bungeni na Mbunge wa Mkanyageni, Mohamed Habib Mnyaa (CUF), wakati akichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia. 

“Mashine hiyo pia ilishawahi kupitishwa paka, akafa hapohapo kutokana na ukali wa mionzi yake...hili ni tatizo tena wanaopitishwa ni wafanyakazi Waswahili (Watanzania) na Wazungu hawapitishwi” 

Gazeti la Mwananchi Leo. 
Makachero wamfuata dalali wa Rada 
HATIMAYE Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba amezungumzia taarifa za kukamatwa kwa dalali anayetuhumiwa kufanikisha kashfa ya ununuzi wa rada, huku kukiwa na taarifa kuwa wapelelezi wa Tanzania wako Uingereza kufuatilia taratibu za kumrejesha nchini. 

Manumba amekuwa akichelea kuzungumzia taarifa za kufuatiliwa kwa mtuhumiwa huyo, Sailesh Vithlan anayedaiwa kufanikisha ununuzi huo tata wa rada yenye thamani ya pauni 28 milioni, lakini jana alidokeza kuhusu uwezekano wa mtuhumiwa huyo kurejeshwa nchini. 

â€Å“Huwezi kusema ataletwa lini, kinachofanyika ni taratibu za kisheria siyo rahisi kusema lini kwani pia kuna taratibu za kimahakama,â€� alifafanua Kamishna Manumba alipoulizwa kwamba Vithlan atarejeshwa lini. 

Manumba alifafanua kuwa katika kushughulikia suala la mtuhumiwa huyo halina budi kuna ulazima wa kuangalia taratibu nyingine za kisheria, ikiwa ni pamoja na za kimahakama. 

Polisi wabaini wizi mkubwa kwenye ATM 
WIMBI la wizi wa fedha kwenye akaunti za wateja kupitia mashine za ATM sasa umefikia kiwango cha kutisha baada ya polisi kukamata watu wawili raia wa Bulgaria waliokuwa wanatumia chombo maalumu kunasa namba za siri za kadi na kuchota fedha kirahisi. 

Jeshi la Polisi, Kanda ya Dar es Salaam limesema watu hao wanatuhumiwa kuchota kiasi cha Sh70 milioni kutoka kwenye akaunti za wateja wa benki mbalimbali ambao huchukua fedha zao kwenye mashine hizo za ATM. 

Kwa mujibu wa polisi, kifaa hicho kina uwezo wa kunakili taarifa za kadi za ATM, ikiwa ni pamoja na namba za siri ambazo huwawezesha wezi kuingia kwenye mashine na kuchota kiasi cha juu cha fedha kulingana na kiwango cha ukomo wa mashine hizo.

Monday, July 20, 2009


Makocha waangalie wazawa zaidi - Mgosi
Mussa Hassan Mgosi mshambuliaji wa timu ya soka ya Simba amesema licha ya changamoto iliyopo sasa katika soka la Tanzania kutokana na kuwa na wachezaji wengi wa kigeni, amewataka makocha kutoa kipaumbele zaidi kwa wachezaji wazawa. Mshambuliaji huyo wa Simba anayekwenda Norway kuungana na Henry Joseph, alisema si jambo jema kwa makocha kupapatikia wachezaji kutoka nje ya nchi na hasa wenye viwango vidogo. "Makocha waangalie sana wachezaji wazawa, si...
Mussa Hassan Mgosi mshambuliaji wa timu ya soka ya Simba amesema licha ya changamoto iliyopo sasa katika soka la Tanzania kutokana na kuwa na wachezaji wengi wa kigeni, amewataka makocha kutoa kipaumbele zaidi kwa wachezaji wazawa. 

Mshambuliaji huyo wa Simba anayekwenda Norway kuungana na Henry Joseph, alisema si jambo jema kwa makocha kupapatikia wachezaji kutoka nje ya nchi na hasa wenye viwango vidogo. 

“Makocha waangalie sana wachezaji wazawa, si kwa sababu ni mchezaji wa kulipwa kutoka nje amesajiliwa basi atacheza tu hata kama hana kiwango kumzidi mchezaji wa hapa nyumbani,” alisema. 

“Tunajua kuwa kuja kwa wachezaji wa kigeni ni changamoto kubwa kwetu katika ligi yetu, lakini usawa uangaliwe zaidi, kuna wachezaji wa hapa nchini ni wazuri kuliko wa kigeni, lakini hawapewi nafasi, kwa sababu tu kuna wachezaji kutoka nje,” alisema Mgosi. 

“Mfano ligi ya msimu uliopita kulikuwa na wachezaji wengi tu wa kigeni, lakini baadhi yao tu ndio waliofanya vizuri ila wengi wao hatukuona mchango wao katika timu, na badala yake wachezaji wa hapa nchini wengi ndio waling’ara,” alisema Mgosi. 

Alisema pia wachezaji wazawa itabidi wajitume ipasavyo kukabiliana na changamoto hiyo kama kweli wana nia ya kupata namba katika kikosi cha kwanza. 


Usiku wa kuamkia leo mtoto wa kike wa MB Dogg amefariki dunia, mtoto huyu alikuwa anaitwa Suhaila Mohamed na alikuwa na umri wa miaka 7...atazikwa leo saa 6 mchana.

Thursday, July 16, 2009


Government on the dock

My spies tell me that the government has been placed on the dock and asked to explain the obvious collusion between the waheshimiwa and the country’s grand corruption
I hear some 50 non-governmental organizations, under the umbrella of the Feminists Activists Coalition (FemAct), have met to deliberate on recent corruption outrages committed with the tacit nod of the government, they claim. Later they released a hard hitting statement which my spooks on-passed to me.

They were openly outraged; “Stories of syndicated grand corruption in the country are horrifying, and force us to draw the conclusion that the Tanzanian state has been hijacked!” The NGOs claim that the state has been bought wholesale and is dancing to the tunes of a few powerful moguls working as one in a powerful corruption network and syndicate to the detriment of the majority of Tanzanians.

“FemAct recognizes syndicated and grand corruption as all private gain-motivated abuse of public office, plunder of public property and lying in the name of ‘nationalisation’, corruption in the electoral processing, lack of transparency in public contraction processes, (meaning public procurement, public investment, privatization), budget execution without consideration of national priorities, discriminatory enforcement of laws and regulations and disobedience of public leadership ethics.” the hard hitting statement said.

FemAct demanded that government immediately and without excuse to prosecute all persons suspected all persons suspected of grand corruption cases and dismantle their corruption networks.

The held the government responsible to implement wholly the Parliamentary resolution on Richmond and provide credible a public restatement on all grand corruption scandals currently in public debate.

FemAct also demanded that the government disclose all existing investment contracts for public access and scrutiny and ensure state function enforcement organs especially the cops, The Directorate public prosecution, the Prevention and Combating of Corruption Bureau (PCCB) and the National Security (intelligent services) conduct their respective business in an accountable manner under strict adherence to professional ethics and expected competences.

The NGOs sounded genuinely angry. But will the government listen to such demands? Few believe it will. So far it has displayed a thick skin and pooh poohed the countrywide protests.

Most analysts expressed strong doubts if the government will listen this time.. “These guys are amazing. They are busy fiddling while Rome is burning. Either that is being tough or foolhardy.” One analyst sighed resignedly in the city recently.

Wednesday, July 15, 2009


Introducing Ruka Wear
Ukibahatika kukutwa umevaa T Shirts ya Ruka mjini basi unabahati ya kupata T shirts nyingine bure. Hayo yameongelewa na Mkurugenzi wa Ruka wakati akiongea na Dar411 katika kuwashukuru wateja wake wote waliofanikisha kufika na kunununa nguo za Ruka kwenye banda lao kipindi chote cha maonyesho ya sabasaba. "Huu ni....

Ukibahatika kukutwa umevaa T Shirts ya Ruka mjini basi unabahati ya kupata T shirts nyingine bure.

Hayo yameongelewa na Mkurugenzi wa Ruka wakati akiongea na Dar411 katika kuwashukuru wateja wake wote waliofanikisha kufika na kunununa nguo za Ruka kwenye banda lao kipindi chote cha maonyesho ya sabasaba.

“Huu ni utangulizi tu wa Ruka, lakini siku si nyingi tutafanya mengi zaidi kwa wateja wetu, kuna kofia zinakuja, kuna jeans yote hiyo ni muendelezo wa kuikuza Ruka ili ije kuwa chata kubwa kabisa kama zilivyo Sean John na nyingine” alisema Mkurugenzi huyo.

Ukitaka kupata Pamba za Ruka wakati wowote usisite kupiga simu number 0717 74 95 81 utaletewa mpaka Mlangoni kwako.web www.rukapamba.blogspot.com






Sunday, July 5, 2009






SABASABA 2009
Karibuni sana katika blog ya nipe habari leo nakupa habari kuhusu sabasaba jinsi wananchi wanavyo endele kunufaika na maonesho haya ya biashara nilijaribu kuwaoji wadau wanaonaje sabasaba ya mwaka huu wadau wananiambia yani imeandaliwa vizuri sana hata mabada yamepngwa vizuri hata utaratibu ni mzuri.


Thursday, July 2, 2009


Press Release

In essence of this trip and Vancouver whitecaps visit to Tanzania Lz enterprise with the endorsement and support from the government fulfilled her objectives in promoting tourism and sports development in Tanzania, LZ ENTEERPRISE wouldn’t fulfill her goals if it wasn’t for the support of the government at large the ministry of sports and culture, TFF, Tanzania tourist board, TANAPA, Ngorongoro conservation, NMB, TBC Serengeti breweries, Quality group, Azam FC, Sea Clif Hotel, Sopa lodges and other individual actors who regardless of other responsibilities they worked hand on hand with us to make all things happen.

Today, two amongst four players who are supposed to go for a trial in Canada are ready, and with the request of the management of the Vancouver whitecaps Nadir Haroub Ali (Canavaro) and Nizar Khalifan will be the first to join the team in Canada for trial followed by others upon the mention and the time table of the team. Whitecaps Vancouver. The two players will be departing any time from today.

We are greatly honored to be as a gate way through for this sports development in Tanzania but it should be noted that it is through good relationship and friendship between the Government of Tanzania and Canada that the visitation of Vancouver was a success and so this trial opportunity to our players too

LZ ENTERPRISE BACKGROUND

LZ Enterprise is based between the U.S. and Tanzania, dedicated to sports development through international exchange, youth development, and the universal game of football. In 2005, LZ Enterprise produced the Tanzania Soccer Summit hosting the Seattle Sounders in Tanzania for international friendship, football development, as well as introducing sports-tourism to Tanzania’s tourism sector. LZ Enterprise worked with the TZ Tourist Board to produce film doc, Discover Tanzania, which can be currently viewed on their website at: http://www.tanzaniatouristboard.com/pages/ttb_video.php.

LZ Enterprise, most recently, signed a letter of intent with the Govt. of Tanzania to initiate a (2.5 mill USD) nationwide sports development programme in Tanzanian schools: http://dailynews.habarileo.co.tz/features/index.php?id=8822

e are currently doing an overhaul on the LZ Enterprise website, but in the meantime there is a presentation from the Whitecaps visit at: www.sakulsky.com/tanzania

ABOUT WHITECAPS – www.whitecapsfc.com

Whitecaps team owners, Jeff Mallett – former President and CEO at Yahoo Inc., Greg Kerfoot – CEO of Seagate Software, and Steve Nash – Phoenix Suns guard / current

philanthropist will assist in bringing significant exposure and partnership to not only Tanzanian football, but the greater Tanzanian business community.

NORTH AMERCIAN SOCCER (United Soccer League – Major League Soccer)

The United Soccer Leagues First Division (often referred to as simply, USL-1) is a professional men's soccer league in North America. It is the second tier of soccer in the United States, Canada, and Puerto Rico league pyramid behind Major League Soccer. There are 11 teams managed by the United Soccer Leagues (USL).

ABOUT MAJOR LEAGUE SOCCER

Headquartered in New York City, Major League Soccer is the top-flight professional soccer league in the United States and features many stars from the U.S. and around the world. The League's 14th season kicks off April 7, 2009. The 13 teams in MLS are: the Chicago Fire, Colorado Rapids, Chivas USA, Columbus Crew, D.C. United, FC Dallas, Houston Dynamo, Kansas City Wizards, Los Angeles Galaxy, Red Bull New York, New England Revolution, Real Salt Lake and Toronto FC.

MLS was founded in 1993 as part of the bid for the United States to host the 1994 FIFA World Cup. The first season took place in 1996 beginning with 10 teams. Seasons run from late March or early April to November, with teams playing 30 regular season games each. Eight teams from the league compete in the post-season MLS Cup Playoffs, which culminate in MLS Cup

Media contact:

Rahim Zamunda Kangezi

zamunda@lzenterprise.net

+255-713-255-614

+1206-755-0332